Watendaji wa Wizara ya Ardhi ni sehemu ya tatizo


Magazeti ya leo yana habari kuhusu kusimamishwa kwa baadhi ya watendaji waandamizi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutokana na sakata la kumilikisha eneo la TAZAMA kwa mfanyabiashara binafsi wa mafuta kinyume cha taratibu.

Jimbo la Kigamboni ni eneo ambalo liko karibu na kitvu cha Jiji la Dar Es Salaam, kutokana na sababu hii, eneo hili limekuwa ni kimbilio la watu wengi kwa sasa.

Mnamo mwaka jana kipindi cha Pasaka, wakazi wa kata ya Tungi walishuhudia ujenzi wa uzio uliokuwa unafanyika usiku na mchana chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi. Kwa jitihada za uongozi wa wananchi katika eneo hili ujenzi huo ulisimamishwa.

Sakata hili limekuja kujitokeza tena majuzi baada ya uongozi wa TAZAMA kulalamika kuhusu kuingiliwa eneo lao.  Baada ya uchunguzi wa ndani, umeonyesha kuwa waliohusika kupindisha sheria na kumilikisha eneo la TAZAMA kinyume cha sheria kwa mwekezaji walikuwa watendaji waandamizi wa Wizara ya Ardhi.

Sishangai! Kwani watendaji wa Wizara ya Ardhi wamekuwa ni vinara wa migogoro ya ardhi katika Jimbo la Kigamboni.

Si siri, watendaji wa Wizara walimega na kujigawia viwanja vyingi katika Mradi wa viwanja 20,000 katika eneo la Kisota na Kibada. Hadi hivi sasa wauzaji wakubwa wa viwanja maeneo haya ni watendaji wa Wizara ya Ardhi. Hadi hivi sasa Wizara inapata kigugumizi kufanya mapitio (audit) ya zoezi la viwanja 20,000 pamoja na kulipigia kelele sana suala hili.

Watendaji wa Wizara ya Ardhi wakiwa na wawekezaji bandia wamekuwa wakienda moja kwa moja kwa wananchi na kuwatisha, kuwapokonya ardhi yao na kuwamilikisha wawekezaji bandia bila kufuata taratibu na kuwalipa wananchi fidia chini ya viwango vya Serikali.

Hata mradi wa Mji Mpya wa Kigamboni, kuna mapungufu mengi ambayo yanayosabishwa na watendaji wa Wizara kupindisha sheria na kuweka maslahi binafsi mbele.

Natumai Wizara itachukua nafasi hii kujitathmini, kuondoa watumishi ambao si waaminifu na kurejesha heshima na imani kwa wananchi.

Posted in Uncategorized | Tagged , , , | Leave a comment

Bomoa bomoa Mtaa wa Minondo, Somangila, Kigamboni


DSCN0506Hivi majuzi nyumba zipatazo 34 za wakazi wa eneo la Minondo, Amani Gomvu, Somangila walivunjiwa ili kupisha ujenzi wa nyumba za vyombo vya ‘ulinzi na usalama’. Kwa mujibu wa wananchi hawa walivamiwa saa kumi alfajiri na kuamriwa kutoka nje ya nyumba zao ili kupisha zoezi la ubomoji. Wananchi hawa wanadai hawakupewa notisi kuhusu zoezi la ubomoaji .

Kimsingi, wananchi hawa hawapingi mradi huu, ila wanalalamikia kubomolewa nyumba bila kulipwa fidia na wengine kupewa kiwango kidogo cha fidia ambacho ni tofauti na viwango vya soko.

DSCN0507Moja ya nyumba 34 zilizobolewa.

DSCN0508

Nilifuatilia maelezo ya waathirika kuhusu sakata la bomoabomoa.

DSCN0510

Nikipitia baadhi ya vielelezo walivyokuwa navyo waathirika.

DSCN0516

Nyumba ya kisasa ya vyumba vitano ilibomolewa. Wahusika hawakupewa nafasi ya kukoa mali zao.

DSCN0517

Nikimpa pole mmoja wa waathirika aliyebomolewa nyumba yake. Bw huyu ndiye mmiliki wa nyumba hapo juu.

Posted in Uncategorized | 4 Comments

Shughuli za kichama kata ya Charambe


image
Siku ya Jumanne tarehe 16 Aprili 2013 ilikuwa ni maalumu kwa kutembelea na kuongea na Vijana katika kata ya Charambe. Tulijadiliana mambo pamoja na kushauriana mambo mengi ya kimaisha. Nilifurahishwa kuona vijana wengi walikuwa na mwamko mzuri kwa CCM. Pichani: Nikikabidhi kadi za Umoja wa Vijana kwa wanachama wapya Wa UVCCM.
image
Zoezi hili liliambatana na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wanaoishi kwenye Kata ya Charambe. Siku hiyo nami nilipata kujua kwamba Mkubwa Fella wa TMK Wanaume ni mdau na mpigakura. Bw Fella alinijulisha kuwa Mhe. Temba, Chege, Juma Nature, Dogo Asley wote ni wadau Wa Jimbo la Kigamboni. Pale burudani iliponoga ilibidi kuingia uwanjani.
image
Moja ya mashina matano ya wakereketwa niliyozindua siku hiyo.
image
Shughuli ni watu na kazi na dawa.

Posted in Uncategorized | 2 Comments

Maandamano ya CCM na Chadema yazuiwa


Maandamano ya CCM na Chadema yazuiwa

Image | Posted on by | Leave a comment

Taj Mahal


Taj Mahal
Jengo hili lilijengwa na Mfalme Shah Jahan kama kumbukumbu ya mke wake kipenzi na lilichukua zaidi ya miaka arobaini kukamilika.
Eneo hili ni maarufu sana. Kilichonifurahisha leo ni kuona Wahindi wengi wanafanya utalii Wa ndani kwa kujitokeza kwa wingi kutembelea kumbukumbu hii.

Posted in Uncategorized | Leave a comment

Ziara ya India


20130321-185629.jpg
Baadhi ya Wabunge kutoka Afrika wakifuatilia maelezo toka kwa Meneja Mkuu Wa Taasisi ya Serikali ya India inayojihusisha na kutoa mafunzo na kuwawezesha wajasiriamali wadogo wadogo.
20130321-185637.jpg
Nikiwa na Wabunge toka Zambia na Zimbabwe.

Posted in Uncategorized | Leave a comment

Ubalozini Delhi, India


Ubalozini Delhi, India

Niko nchini India nikiwakilisha Bunge la Tanzania kwenye kongamano la Wabunge vijana toka Bara la Afrika lililoandaliwa na Serikali ya India.
Wabunge wengine wanaoshiriki toka Tanzaniani Mhe. Namelok Sokoine (MB) na Mhe. Saidi Mussa Zuberi (MB). Taarifa ya ziara nitaitolea maelezo katika andiko jingine.
Jana tulipata fursa yakutembelea Ubalozi wetu hapa New Delhi na kupata mapokezi mazuri.
Mhe. Balozi alitupatia taarifa kuhusu mahusiano kati ya Tanzania na India. Mafanikio katika falsafa ya diplomasia ya kiuchumi ni pamoja na kukua kwa biashara baina ya nchi hizi mbili kutoka USD 1,230 million mwaka 2008/9 hadi kufikia 1,729.4 mwaka 2010/2011. Vilevile Serikali ya India imekuwa na mchango mkubwa katika sekta ya kilimo na katika mafunzo ya wataalamu mbalimbali chini ya mpango India Technical and Economic Cooperation (ITEC).
Picha: Mstari Wa mbele kuanzia kushoto: Mhe Namelok Sokoine, Mdau, Mhe. Balozi John Kijazi, Mhe. Saidi Zuberi, Dr Kheri Goloka.
Mstari Wa nyuma toka kushoto: Bi Fadhila Mwindadi, Bi Felistas Mwalukasa, Bi Leluu Abdalla, Bi Badriya Kiondo na Bw Yahya Mhata

Image | Posted on by | Tagged , , | Leave a comment