Ujenzi wa daraja la Kigamboni

Nimepokea kwa furaha kubwa sana taarifa ya uwekaji saini mkataba wa ujenzi wa daraja kati ya mkandarasi na NSSF.
China Railways Construction Engineering Group kwa ushirikiano na China Major Bridges wameshinda zabuni ya kujenga daraja hili lenye urefu wa mita 680 lenye njia sita kwa gharama za TSh 214.6. Ujenzi utachukuwa miezi thelathini na sita.
Kukamilika kwa barabara hii kutaleta maendeleo na kwa kiasi kikubwa litapunguza gharama za maisha kwa wakazi hao. Katika hili nawapa pongezi Wizara ya Ujenzi kufanya shughuli zake za msingi kwa vitendo. Nawapa pongezi pia NSSF kufanikisha mchakato huu kuanza kwa kutoa asilimia 60 ya gharama hizi. Ushiriki wa NSSF ni mfano mzuri wa ushirikishaji wa sekta binafsi (PPP).
Wananchi wa Kigamboni tutatoa ushirikiano kuhahakisha daraja hili linakamilika katika muda uliopangwa.
Mungu ibariki Tanzania Mungu Ibariki Kigamboni

About Dr Faustine Ndugulile

#Medical Doctor #Microbiologist # Public Health Specialist #Politician #African #Proud Tanzanian
This entry was posted in Uncategorized. Bookmark the permalink.

3 Responses to Ujenzi wa daraja la Kigamboni

  1. Fausta says:

    This is great news; thanks for sharing.

    Like

  2. UKAMILIKAJI WAKE UTAKUWA NI MFANO, ALAMA NA ISHARA YA UTHUBUTU KWA WATANZANIA WOTE, ” TUKITAKA TUNAWEZA”

    Like

Leave a comment